Tuesday, November 26, 2024

 

 
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimehitimisha kampeni zake za uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika kata ya Ruvuma, Manispaa ya Songea, mkoani Ruvuma.

Hafla ya kufunga kampeni hizo imefanyika leo Novemba 26,2024 ikihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama hicho, wakiongozwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mohamed Aboud.

Katika hotuba yake, Aboud amewataka wakazi wa mkoa huo kuchagua viongozi wazuri watakaoweza kutatua changamoto na kero za wananchi, akisisitiza kuwa viongozi bora ni wale wanaotokana na CCM.


Aidha, Aboud amekubali mapendekezo ya Mbunge wa Viti Maalumu, Mariamu Nyoka, na Jackline Ngonyani (Msongozi), akisema yuko tayari kushirikiana nao kutatua changamoto mbalimbali, hasa za wanawake wa mkoa wa Ruvuma.


Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unatarajiwa kufanyika Novemba 27,2024


 
YANGA imeanza vibaya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika ikifungwa mabao 2-0 nyumbani dhidi ya Al Hilal kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Swali kubwa lililoibuka baada ya matokeo hayo ni, tatizo nini? 
 
Mabao ya Adama Coulibaly dakika ya 63 na Yasir Mozamil (dk 90) yaliitibulia Yanga ambayo haikuwa imeruhusu idadi hiyo ya mabao tangu irejee katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu uliopita baada ya takriban miaka 25.
 
Mabao hayo yalitokana na safu ya beki ya Yanga chini ya mabeki wa kati, Ibrahim Bacca na Dickson Job kutokuwa makini kuwazuia nyota wa Al Hilal. 
 
Pia washambuliaji wa Yanga walishindwa kuwa na utulivu kwenye robo ya mwisho ya uwanja kutokana na namna timu hiyo imekuwa ikijenga mashambulizi. 
 
Hata hivyo, msimu huu Yanga ilianza vizuri michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na hatua za awali hadi inafuzu makundi ilifunga mabao 17 bila ya nyavu zake kutikiswa. 
 
Novemba 15 mwaka huu, Yanga ilifanya mabadiliko ya benchi la ufundi ikimwondoa Kocha Mkuu, Miguel Gamondi na msaidizi wake Moussa N’Daw, nafasi zao zikachukuliwa na Sead Ramovic na Mustapha Kodro. 
 
Leo ndiyo kilikuwa kibarua cha kwanza kwa makocha hao ambao wameanza kwa kichapo cha aibu kilichoibua maswali mengi. 
 
Katika dakika 45 za kwanza za mchezo huo wa Kundi A, Yanga ilionekana kuanza kwa kasi huku Al Hilal ikiwa taratibu lakini kadri muda ulivyokuwa unakwenda mambo yalikuwa yakibadilika. 
 
Prince Dube ambaye leo alikabidhiwa mechi hiyo maalum ikipewa jina lake, alipata nafasi nyingi za kufunga lakini umakini mdogo ukaikosesha timu yake mabao. 
 
Dakika hizo 45 za kwanza, Dube alikosa nafasi tatu za wazi ambao kama angekuwa makini basi angeifungia timu yake.
Bado kocha Ramovic atakuwa na kazi ya kufanya kuhakikisha wachezaji wake wanashika falsafa zake akitaka kuona timu wanacheza soka la kasi lakini mbele kwenye umaliziaji. 
 
Washambuliaji wa Yanga walishindwa kuwa na utulivu kwenye robo ya mwisho ya uwanja kutokana na namna timu hiyo imekuwa ikijenga mashambulizi. 
 
Kukosa kwa nafasi hizo kumeendelea kuibua maswali ambapo Dube msimu huu amekuwa hana wakati mzuri kitakwimu ukiachana na mabao matatu aliyofunga hatua ya awali katika michuano hiyo, hana bao lingine. 
 
Mbali na Dube kukosa nafasi hizo, lakini kukosekana kwa Khalid Aucho eneo la kiungo mkabaji imeonekana kuitesa zaidi Yanga na iliamua kumtumia Mudathir Yahya aliyesaidiana na Duke Abuya. 
 
Viungo hao walionekana kushindwa kupandisha mashambulizi mbele na kuwaacha viungo wa Al Hilal kutawala eneo hilo licha ya kwamba Yanga ndiyo iliutawala mchezo kwa jumla kitakwimu za umiliki wa mpira. 
 
Nguvu kubwa waliyokuwa nayo Al Hilal ilikuwa kutumia pembeni kufanya mashambulizi yake hasa upande wao wa kulia na Steven Ebuela alionekana kumsumbua beki wa kushoto wa Yanga, Nickson Kibabage. 
 
Hata bao la kwanza lililofungwa na Coulibaly alitumia udhaifu wa upande huo wa Yanga, pia lile la pili lilipitia upande wa kulia wa Yanga. 
 
Kwa ujumla, wachezaji wa Yanga katika mchezo wa leo walicheza kwa morali ya chini iliyowafanya kupoteza mchezo huo ikiwa ni mara ya pili mfululizo mbele ya Al Hilal. 
 
Mara ya mwisho timu hizo zilikutana Oktoba 16, 2022 katika mchezo wa mtoano wa Ligi ya Mabingwa Afrika uliochezwa nchini Sudan na wenyeji Al Hilal kushinda 1-0. Kabala ya hapo, Oktoba 8, 2022 jijini Dar es Salaam, matokeo yalikuwa sare ya 1-1.
Ushindi huo unamfanya Kocha Florent Ibenge wa Hilal kuendelea kufurahia kukutana na Yanga kwani hajawahi kupoteza dhidi yao akishinda mara mbili nyumbani na ugenini na kutoa sare mara moja katika mechi tatu walizokutana. 
 
Kocha wa Al Hilal, Florent Ibenge amesema: “Yanga ni timu kubwa, tulichokifanya ni kucheza kwa tahadhari, kipindi cha kwanza hakutuwa na mikakati ya ushindi, lakini kipindi cha pili ndiyo tulihitaji ushindi.
“Mpango huo ulikuwa ni kuhakikisha tunashambulia huku tukilinda lango letu kwa tahadhari kubwa baada ya kuona kipindi cha kwanza wapinzani wameshindwa kutufunga.”
Kocha Ramovic amesema: “Inaumiza, nimeanza namatokeo mabaya ya kipigo, kama timu kubwa tunarudi kujipanga na mechi zijazo, tunajua tuna mechi nyingi mbele, tutahamikisha tunafanya vizuri.
“Ukiangalia utimamu wa wachezaji upo chini kulinganisha na aina ya soka ninalotaka kucheza ni vitu tofauti hivyo kuna kazi ya kufanya kuhakikisha mambo yanakuwa mazuri. 
 
“Huu ni mwanzo, bado kuna mechi zingine za kucheza ambapo tuna wakati wa kusahihisha makosa ambayo tumeona leo yametokea ikiwemo kushinda kuzitumia vizuri nafasi tulizotengeneza.” 
 
Licha ya Yanga kupoteza mchezo huo, inaweza kurudi na kufanya vizuri baada ya wapinzani wengine wa kundi lao, TP Mazembe na MC Alger kutoka 0-0 na kufanya msimamo kusomeka hivi; Al Hilal pointi 3, MC Alger (1), TP Mazembe (1) na Yanga (0). 
 
Baada ya mchezo wa leo, Novemba 30 mwaka huu Yanga itakuwa ugenini kucheza na Namungo ukiwa ni mwendelezo wa Ligi Kuu Bara, kisha Desemba 6, itaenda Algeria kupambana na MC Alger iliyofungiwa na Caf mashabiki wake wasiingie uwanjani.


 
 
Aliyekuwa kocha wa makipa wa timu ya Simba, Muharami Sultani (40) na wenzake wanaendelea kusota rumande kwa siku 736 kutokana na upelelezi wa shauri linalowakabili kutokamilika.



Sultan na wenzake watano wanakabiliwa na mashtaka manane yakiwemo ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroin zenye uzito wa kilo 34.89 pamoja na kutakatisha fedha. 
 
Kwa mara ya kwanza washtakiwa hao walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisitu, Novemba 21, 2022 na kusomewa mashtaka yao.
 
Hata hivyo, tangu wafikishwe mahakamani hapo siku hiyo hadi leo Novemba 26, 2024, washtakiwa hao wamefikisha siku 736 sawa na miaka miwili na siku tano wakiwa rumande. 
 
Licha ya upelelezi wa kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 71/2022 kutokamilika, pia washtakiwa hao wanaendelea kusota rumande kutokana na mashtaka yanayowakabili kutokuwa na dhamana kwa mujibu wa sheria.
Pia mashtaka ya kutakatisha fedha hayana dhamana kwa mujibu wa sheria. 
 
Hata hivyo, leo wakili wa Serikali Frank Rimoy aliieleza mahakama hiyo, kuwa upelelezi wa shauri hilo bado unaendelea, hivyo Serikali inaomba mahakama ipange tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa. 
 
Hakimu Mkazi Mwandamizi, Godfrey Mhini, aliahirisha shauri hilo Desemba 10, 2024 kwa ajili ya kutajwa na washtakiwa wapo rumande kutokana na kesi hiyo kutokuwa na dhamana. Kesi hiyo imesikilizwa kwa njia ya video huku washtakiwa wakiwa rumande. 
 
Mbali na Sultani, washtakiwa wengine ni mmiliki wa kituo cha Cambiasso Sport Academy kilichopo Tuangoma, Dar es Salaam, Kambi Zubery Seif; Said Matwiko mkazi Magole na Maulid Mzungu maarufu mbonde (54) mkazi wa Kisemvule, Dar es Salaam ambaye ana undugu na mtuhumiwa Muharami. 
 
Wengine ni John John maarufu Chipanda (40) mkazi wa Kitunda ambaye kazi yake ilikuwa ni kutafuta vijana wenye vipaji na kuwapeleka Cambiasso Sport Academy pamoja na Sarah Joseph. 
 
Miongoni mwa mashtaka yanayowakabili ni kuongoza genge la uhalifu shtaka linalowakabiliwa watu wote ambapo inadaiwa tarehe tofauti kati ya mwaka 2016 na Novemba 4, 2022 katika maeneo tofauti na ndani ya mikoa ya Dar es Salaam na Pwani washtakiwa hao waliongoza genge la uhalifu kwa lengo la kusafirisha dawa za kulevya aina ya Heroin Hydrochloride.
Shtaka la pili inadaiwa kuwa Oktoba 27, 2022 katika eneo la Kivule wilaya ya Ilala mkoani Dar es Salaam washtakiwa hao kwa pamoja walikutwa wakisafirisha dawa za kulevya aina ya Heroin zenye uzito wa kilo 27.10. 
 
Vile vile, Novemba 4, 2023 washtakiwa, Zuberi, Zungu na Mtwiko katika eneo la Kamegele wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani, walikutwa wakisafirisha dawa za kulevya aina ya Heroin zenye uzito wa kilo 7.79. 
 
Katika shtaka la nne, tano, sita na saba ambayo ni ya utakatishaji fedha yanayomkabili mshtakiwa Kambi inadaiwa kuwa Aprili 15, 2021 katika wilaya ya Ilala mkoani Dar es Salaam alinunua magari manne aina ya TATA yenye jina la Safia Group of Companies LTD huku akijua mali hizo zilipatikana kwa kosa la kuongoza genge la uhalifu. 
 
Katika shtaka la nane inadaiwa kuwa Aprili 20,2021 mshtakiwa Kambi alinunua gari aina ya TATA yenye jina Safia Group of Companies LTD akijua mali hiyo ilipatikana kwa kosa la kuongoza genge la uhalifu.




JESHI la Polisi mkoani Shinyanga,limewataka wananchi mkoani humo, kuwa siku ya kesho wajitokeze kwa wingi kupiga kura kuchagua viongozi wa serikali za mitaa,kwamba amani na usalama utakuwepo.

Hayo yamebainishwa leo Novemba 26,2024, na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Janeth Magomi, wakati akizungumza na vyombo vya habari.

Amesema kesho novemba 27 ni siku ya uchaguzi wa viongozi wa Serikali za Mitaa, kuwa Jeshi hilo limejipanga vyema kuhakikisha usalama kwa wananchi wote unakuwepo, kuanzia majumbani na kwenye vituo vya kupigia kura, na kuwasihi wananchi kwamba wajitokeze kwa wingi kushiriki kwenye uchaguzi huo sababu amani ya kutosha itakuwepo.

“Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, tunatoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uchaguzi wa serikali za mitaa, kwani tumejipanga vyema kuhakikisha usalama kwa unakuwepo muda wote kuanzia majumbani na kwenye vituo vya kupigia kura,”amesema Magomi.

Aidha, amesema Jeshi hilo pia limewakamata wahamiaji haramu Saba ambao ni Raia wa Burundi,katika kijiji cha Nyamilangano halmashauri ya Ushetu wilaya Kahama, kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha Sheria, na wamewapeleka katika ofisi za uhamiaji kwa hatua zaidi za kisheria.

Amesema pia , wamekamata watu 51 kwa tuhuma za wizi pamoja na vielelezo mbalimbali zikiwamo bangi kilo 10, pikipiki Tisa, Pombe aina ya Moshi Lita 15,Godoro Nne, Container mbili za bati, mashine tatu za bonanza, gari likiwa na nondo 130, binding wire 11,mifuko 100 ya saruji, simu mbili, redio Saba, kabati,friji na kitanda kimoja.

Amesema kupitia kikosi cha usalama barabarani, wamefanikiwa kukamata jumla ya makosa 7,920, ambapo makosa ya gari ni 5,615, bajaji na pikipiki ni 2,305, huku wakimfikisha mahakamani dereva mmoja kwa kosa la kuendesha gari akiwa amelewa na kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja

Unordered List

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua. Ut enim ad minim veniam, quis nostrud exercitation test link ullamco laboris nisi ut aliquip ex ea commodo consequat.

Duis aute irure dolor in reprehenderit in voluptate another link velit esse cillum dolore eu fugiat nulla pariatur.

Sample Text

Blog Archive

Powered by Blogger.

ABOUD AFUNGA KAMPENI ZA UCHAGUZI CCM RUVUMA

    Chama cha Mapinduzi (CCM) kimehitimisha kampeni zake za uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika kata ya Ruvuma, Manispaa ya Songea, mkoan...

Search This Blog

Find Us On Facebook

Random Posts

Social Share

Flickr

Events

Text-Widgets

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua. Ut enim ad minim veniam, quis nostrud exercitation test link ullamco laboris nisi ut aliquip ex ea commodo consequat. Duis aute irure dolor in reprehenderit in voluptate another link velit esse cillum dolore eu fugiat nulla pariatur.

Sponsor

Recent comments

Recent Comments

?max-results=10">Gallery
');
    ?orderby=published&alt=json-in-script&callback=mythumb\"><\/script>");

Popular Posts

Popular Posts

Recent Posts

Header Ads

Text Widget